Kenya yachagua kikosi cha kuteka dunia mbio za nyika

MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.

Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.

Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.

Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.

“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.

Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.

Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).

Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.

Connexion utilisateur

Commentaires récents

  • Ne pas "hiérachiser les souffrances", disent-ils...

    SOUSE

    Albè

    03/04/2026 - 09:35

    An plis, sé jounalis, entélektiel, politisien, artis-nou an, sé an bann Sousè ! Lire la suite

  • Controverse Mémona Hintermann-Afféjee : « Je porterai plainte si le lycée est débaptisé »

    Le hasard n'exite pas !!

    yug

    02/04/2026 - 15:16

    MH à CNews ?? Pas l'effet du hasard !! Lire la suite

  • Une Tunisienne à la tête d’Orly : l’ascension d’Imène Souid à Paris

    LOOOL !

    Albè

    02/04/2026 - 07:08

    Donc le type est esclave et c'est à lui que l'on confie le soin de lancer l'appel de la toute nou Lire la suite

  • Une Tunisienne à la tête d’Orly : l’ascension d’Imène Souid à Paris

    Allah Akbar ? (Dieu est il si "grand" que ça ?)

    yug

    01/04/2026 - 22:25

    Le fait pour un ancien esclave ....noir évidemment (Hi Hi Hi Hi ) d'avoir été le premier muezzin Lire la suite

  • Trois-Ilets : shatta-politics blé-blan-wouj

    EST-CE CELA UN...

    Albè

    30/03/2026 - 17:30

    ...renouvellement politique en Martinique ? Je suis sidéré. Lire la suite

  • Sé li ki té ka mennen avion-an ki dépotjolé 185 manmay-lékol atè Téhéran

    Crime de guerre sanctionné.

    yug

    30/03/2026 - 15:48

    Je ne sais pas si c'est grâce à Allah ,mais c'est bien fait pour sa sale gueule.

    Lire la suite
  • Municipales 2026 en l'île aux fleurs fanées : les mots qu'on n'a pas entendus

    24%...

    Albè

    29/03/2026 - 15:16

    Le bâti (maisons, immeubles, routes etc...) ne couvre que 24% du territoire martiniquais. Lire la suite

  • Municipales 2026 en l'île aux fleurs fanées : les mots qu'on n'a pas entendus

    Superbe article !! Bande d'ordures ,va !!!!!....

    yug

    29/03/2026 - 13:41

    Superbe article ,notamment EN CE QUI CONCERNE LES PLU ET LES TERRES AGRICOLES .Ceci constitue e Lire la suite

  • Maires issus de l'immigration : la fin du « blocage », selon un démographe

    AUTOUR DU POT

    Albè

    29/03/2026 - 06:35

    Vous tournez autour du pot comme une bourrique ivre parce que vous êtes coincé. Lire la suite

  • Maires issus de l'immigration : la fin du « blocage », selon un démographe

    De qui parlez-vous ?

    yug

    28/03/2026 - 22:21

    ...quand vous dites :"En effet, on a vu ce qu'ils ont fait des Juifs à Auschwitz et Dachau." ? Lire la suite