Kenya yachagua kikosi cha kuteka dunia mbio za nyika

MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.

Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.

Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.

Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.

“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.

Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.

Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).

Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.

Connexion utilisateur

Commentaires récents

  • Interdit de rire !...

    Réponse à "Neutralité" ( 3)

    yug

    24/04/2026 - 22:25

    L'holocauste n'est pas un crime contre l'humanité , mais un crime européen contre l'Humanité.
    Lire la suite

  • Tchad : la langue arabe deviendra obligatoire à la prochaine rentrée scolaire

    CIRCONSTANCES ?

    yug

    24/04/2026 - 20:33

    Pourriez vous me préciser les circonstances de l'emploi de ce supplice .Par qui (nom du ou des ma Lire la suite

  • Tchad : la langue arabe deviendra obligatoire à la prochaine rentrée scolaire

    SUPPLICE DU TONNEAU

    Albè

    24/04/2026 - 07:36

    Il vaut mieux avoir été castré que de subir le supplice du tonneau infligé aux esclaves rebelles Lire la suite

  • Tchad : la langue arabe deviendra obligatoire à la prochaine rentrée scolaire

    Et ils le castrèrent...

    yug

    23/04/2026 - 21:44

    Castré comme il l'a été par ses maitres arabes qui en firent après un muezzin ,l' ex-esclave Bil Lire la suite

  • le descendant de Malien bat le descendant de Marocain

    C'EST BIEN BEAU TOUT CELA MAIS...

    Albè

    23/04/2026 - 20:55

    ...les Bumidomiens ils foutent quoi ? Combien de maires élus lors de la dernière élection ? Lire la suite

  • le descendant de Malien bat le descendant de Marocain

    La réponse à la question finale este"OUI"! Dans toutes les...

    Frédéric C.

    23/04/2026 - 19:29

    ...ex- ou pseudo-"ex" métropoles coloniales, il y a une forte immigration des anciennes colonies Lire la suite

  • Tchad : la langue arabe deviendra obligatoire à la prochaine rentrée scolaire

    Hé ZUT !

    Albè

    23/04/2026 - 07:41

    Les descendants de Bilal vont encore faire enrager notre "ami" Yug !

    Lire la suite
  • « Je suis raciste et je suis fier » : un homme tire à la carabine sur des enfants « noirs et arabes » en Haute-Loire

    Albè, attention, on risque de confondre...

    Frédéric C.

    21/04/2026 - 19:03

    ...avec le rhum Crassous-de-Médeuil. C’est infâmant pour ce rhum. Lire la suite

  • Le maire de Rivière-Pilote, soutenu par "Péyi-a", ferme RLDM (Radio Lévé Doubout Matinik)

    NB: Ce Maire s’appelle....

    Frédéric C.

    21/04/2026 - 18:48

    ...Jean-François BEAUNOL. Lire la suite

  • « Je suis raciste et je suis fier » : un homme tire à la carabine sur des enfants « noirs et arabes » en Haute-Loire

    YUG EST UN BEKE !

    Albè

    21/04/2026 - 18:23

    On t'a découvert, mon gars ! Lire la suite