MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.
Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.
Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.
Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.
“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.
Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.
Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).
Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.
Tiens c'est bizarre ...je viens de lire une bonne centaine de lignes précédentes sur le racisme Lire la suite
...que c’est "POUR UNE FOIS" que je partageais une opinion de Yug: ça veut dire que la plupart du Lire la suite
Kemi Seba, de son vrai nom Stellio Capo-Chichi, est né en France de parents Beninois... Lire la suite
Sans les crimes de Napoléon en Haiti et des français en Algérie, les nazis ne seraient pas aidés? Lire la suite
Ce qu"Albè dit c'est les blancs empèchent tous critique du génocide de gaza en mettant le génocid Lire la suite
Un Antillais se doit d'être neutre dans le conflit qui oppose Juifs et Musulmans. Pourquoi ? Lire la suite
...je partage votre avis. Lire la suite
...toutes les victimes avec une EGALE DETERMINATION soit on en choisit une__en l'occurence les Ju Lire la suite
Car il existe maints intellectuels tout-à-fait conscients du degré d’abrutissement et de paresse Lire la suite
Il n'y a jamais eu ni Hutus ni Tutsis chez nous : pourquoi en effet se préoccuper du massacre des Lire la suite