Kenya yachagua kikosi cha kuteka dunia mbio za nyika

MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.

Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.

Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.

Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.

“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.

Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.

Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).

Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.

Connexion utilisateur

Commentaires récents

  • L'antisionisme se paie cash, ma belle !

    Albè a kayé .

    tim

    04/01/2026 - 20:33

    L’imprécateur sévissant sous le faux nom de Albè a kayé ....;finies les rodomontades dans lesquel Lire la suite

  • Les négros-franchouillards admirateurs de "Charlie Hebdo" (et du "Canard Enchaîné") en deuil

    PET DE LAPIN

    Albè

    04/01/2026 - 10:44

    BOF ! Les blablas de K.P. Lire la suite

  • Les négros-franchouillards admirateurs de "Charlie Hebdo" (et du "Canard Enchaîné") en deuil

    Albè, sé menm lidé-a mwen ni épi-w...

    Frédéric C.

    04/01/2026 - 10:03

    ...anlè moun ta-la. Lire la suite

  • Les négros-franchouillards admirateurs de "Charlie Hebdo" (et du "Canard Enchaîné") en deuil

    SON NOM ?

    Albè

    03/01/2026 - 18:36

    Mais son nom est connu comme le loup blême contrairement à ce que TIM raconte ! Lire la suite

  • Arrêtez de nous les casser avec vos communiqués "Halte à l'impérialisme américain !"...

    MONROE PA MÒ

    abcx

    03/01/2026 - 18:21

    C'est l'application de la doctrine Monroe dans toute sa splendeur, à laquelle la Martinique, la G Lire la suite