MABINGWA mara 23 wa dunia Kenya wamechagua kikosi cha kudondosha mate kwa makala ya 45 ya Mbio za Nyika za Dunia zitakazofanyika jijini Belgrade, Serbia mnamo Machi 30, 2024.
Agnes Ngetich, Emmaculate Anyango na Lilian Kasait wanaokamata nafasi tatu za kwanza kwa muda bora duniani mwaka huu katika mbio za kilomita 10 za barabarani wa dakika 28:46, 28:57 na 29:32, mtawalia, wako katika kikosi cha taifa cha wakimbiaji 30 kilichochaguliwa katika uwanja wa Chuo cha Mafunzo cha Magereza mjini Ruiru, Kiambu, Jumamosi.
Beatrice Chebet na Ngetich waliozoa dhahabu na shaba mtawalia kwenye Mbio za Nyika za Dunia 2023 nchini Australia, bingwa wa 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Margaret Chelimo pamoja na mshindi wa mbio za nyika za majeshi Cintia Chepngeno wanakamilisha orodha ya washiriki sita watakaotimka kitengo cha 10km cha wanawake. Chepngeno alikosa kumaliza mbio nchini Australia kwa hivyo amepata fursa nzuri ya kujifariji.
Bingwa wa dunia 21km kwenye Riadha za Dunia za Barabarani 2023 Sebastian Sawe ataongoza kikosi cha 10km wanaume kilicho na mfalme wa mbio za nyika kitaifa 2022 Samuel Chebolei, bingwa wa dunia mara mbili mbio za nyika Geoffrey Kamworor pamoja na Gideon Rono, Benson Kiplagat na bingwa wa dunia kitengo cha chipukizi 2023 Ishmael Kipkurui.
“Nilikuwa na matumaini makubwa ya kutwaa tiketi. Mpango wangu wa kutoonekana na kuchomoka zikisalia mita 500 naona ulifanya kazi vizuri,” akasema Sawe anayelenga medali jijini Belgrade.
Reynold Cheruiyot aliyemaliza nyuma ya Kipkurui pamoja na washindi wa dhahabu ya mbio mseto Emmanuel Wanyonyi na Kyumbe Munguti, sawa na Diana Chepkemoi, Emmanuel Wanyonyi na Charles Rotich watapata fursa ya kuimarisha matokeo yao kutoka mwaka 2023.
Timu ya chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20 ya Kenya inajumuisha Sheila Chebet, Deborah Chemutai, Nancy Cherop, Mercy Chepkemoi, Diana Cherotich na Diana Chepkemoi (wanawake kilomita sita) na Samuel Kibathi, Charles Rotich, Mathew Kipkoech, Jonah Erot, Shadrack Rono na Gideon Kipngetich (wanaume kilomita nane).
Cheruiyot, Wanyonyi, Munguti, Virginia Nyambura, Mercy Wanjiru na Purity Chepkirui watashiriki mbio mseto.
Ce célébrissime chant de guerre maori est enseigné (j'espère que c'est encore le cas ) depuis qq Lire la suite
"Confronté à la justice pour son départ en retraite". Lire la suite
D'une mauvaise foi abyssale. Vous faites semblant de ne pas comprendre de quoi il s'agit. Lire la suite
...en France, elle sera lancée par les fascistes-racistes de rue (et armés, circulant en meute). Lire la suite
Super : exigence de partis ,de bandes ,de grouoes ,"d'organisations "et pourquoi pas de mouvement Lire la suite